YANGA YABANWA MBAVU NA MTIBWA SUKARI

   yanga

Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu ya Tanzania bara Yanga, jana wameshindwa kuing'oa vinara wa ligi hiyo Simba baada ya kutoka Sare ya 0-0 na Mtibwa Sugar Jamhuri Mjini Morogoro.

Yanga wangeweza kushinda Mechi hii baada ya kupewa Penati ya Dakika ya 34 lakini Mchezaji wao Simon Msuva akashindwa kuifunga Penati hiyo.

Kwa Matokeo hayo Yanga wanabaki Nafasi ya Pili nyuma ya Simba ambao wako alama 2 mbele yao baada ya Jumamosi kutoka Sare 2-2 na Mbeya City.

Katika Mechi nyingine iliyochezwa jana African Lyon iliitungua Mwadui FC 1-0 .

Ligi hiyo ya Tanzania bara inatarajia kuendelea tena leo Jumatatu Machi 6 kwa mchezo mmoja ambapo Ndanda wanakuchele wanawakaribisha maafande wa Ruvu Shooting.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment