HABARI NJEMA KWA CHELSEA: HAZARD NA TERRY KUSAINI MIKATABA MIPYA.

 Eden Hazard: Nedokážu být takovým kapitánem, jakým je John Terry

Eden Hazard anatarajiwa kubakia Chelsea na kusaini Mkataba Mpya wakati Nahodha wao John Terry akipewa nyongeza ya Mwaka Mmoja.
 
Vigogo wa Spain Real Madrid wamehusishwa na kumnasa Hazard, mwenye Miaka 26, kwa Dau la Pauni Milioni 100 pamoja na kuwapa Chelsea Mchezaji Mmoja lakini Meneja Antonio Conte amekataa na kusisitiza Hazard atabaki Chelsea huku pia Mmiliki wao Roman Abramovich akikataa kabisa kuuzwa kwa Mbelgiji huyo.

Vilevile habari hizi zimedai kuwa hata mwenyewe Hazard hataki kuondoka London ambako Msimu huu amefunga Bao 14 kwa Chelsea na Belgium.

Ripoti hizo pia zimedai Mkataba Mpya wa Hazard hapo Chelsea utampa Mshahara wa £300,000 kwa Wiki.

Wakati huo huo, imefahamika kuwa Nahodha wa Chelsea John Terry amepewa Mkataba Mpya wa kubakia kwa Mwaka Mmoja zaidi ambao utamfanya awe Stamford Bridge kwa Msimu wake wa 20.

Terry, mwenye Miaka 36, aliongezewa Miezi 12 Msimu uliopita baada ya kumalizika Mkataba wake.

Licha ya kuvumishwa Msimu huu ndio mwisho wa Terry, Meneja Conte amesisitiza kuwa Terry bado ni muhimu mno kwa Klabu.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment