WENGER ADOKEZA KUBAKI ARSENAL

>>> >>>>>>>> NI KILIO KWA WADAU WA ‘NI ARSENAL FC SI ARSENE FC’!Tokeo la picha la MASHABIKI WA ARSENAL IMAGE

Arsene Wenger amedokeza kubakia Klabuni Arsenal pale alipotoboa anafanya mipango kwa ajili ya Msimu Mpya lakini akasema Wachezaji Wapya watatua hapo kwa ajili ya Klabu na si yeye.
 
Hata hivyo, Wenger amesisitiza mipango ya Msimu Mpya anaifanya hata kama angekuwa anaondoka mwishoni mwa Msimu huu.

Habari hizi zitakuja kama pigo kubwa kwa Washabiki wanaoshinikiza Wenger aondoke kwa kutoleta mafanikio yeyote tangu 2004 walipotwaa Ubingwa wa England kwa mara ya mwisho.

Wadau hao, wenye Kampeni iliyobatizwa ‘NI ARSENAL FC SI ARSENE FC’, ni wazi watakatishwa tamaa na habari hizi baada ya presha yao kupamba moto hasa baada ya Arsenal kucharazwa 10-2 katika Mechi 2 na Bayern Munich na kutupwa nje ya UCL, UEFA CHAMPIONZ kwenye Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ikiwa ni mara ya 7 mfululizo kufeli Hatua hiyo ya Mashindano hayo.

Inaelekea sasa Wenger atasaini Mkataba Mpya wa Miaka Miwili na moja ya Wachezaji Wapya ambao Wenger amependekeza watue Emirates ni Mchezaji wa Borussia Dortmund, Marco Reus.

Pia inasemekana Wenger sasa anasaka mbadala wa Mesut Ozil na Alexis Sanchez ambao inadaiwa wako mbioni kuhama licha ya Wenger mwenyewe kutamka Juzi wanataka kubaki na mazungumzo nao yanaendelea vizuri.

Akiosha mikono kuwa Wachezaji wapya hutua Arsenal si kwa sababu yake, Wenger ametamka: “Arsenal ni Brandi ya Dunia hivi Leo, inaheshimika Dunia nzima. Jina la Arsenal ni kubwa kupita Jina langu na kuja Arsenal ni muhimu…huji kwa Arsene Wenger..unakuja kwa Arsenal!”

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment