BABA YAKE MZAZI WA PAUL POGBA AFARIKI DUNIA.

Tokeo la picha la POGBA AKIWA NA BABA YAKE IMAGE 

BABA Mzazi wa Kiungo wa Manchester United Paul Pogba amefariki Dunia akiwa na Miaka 79 baada ya kuugua.
 
Fassou Antoine Pogba aliihama Nchi yake Guinea kutoka Afrika na kwenda Paris, France akiwa na Miaka 30.

Mbali ya Paul Pogba, Watoto wake wengine ni Mapacha Florentin na Mathias ambao wote ni Wanasoka.

Wakati Pogba akiamua kuichezea France, Ndugu zake Florentin na Mathias wao waliamua kuiwakilisha Guinea.

Familia ya Pogba ilithibitisha kwa Gazeti la France, Le Parisien, kuwa Mzee Fassou Antoine Pogba, aliekuwa akiugua, alifariki Jana Ijumaa.

Mwaka Jana kwenye Fainali za EURO 2016, Mzee Fassou alionekana Jukwaani Uwanjani akiwa na Wanawe Florentin na Mathias wakimshangilia Paul Pogba akiichezea France walipokutana nae Switzerland.

Mwezi Machi Pogba alitoa Picha kwenye Instagram akisheherekea Siku ya Kuzaliwa ya Baba yake na kuandika:  
'Happy birthday dear Dad, I feel blessed to be your son #pogdaddy #fighter #pogbance.'

             Tokeo la picha la POGBA AKIWA NA BABA YAKE IMAGE

Mzee Fassou alitua France akiwa hana hata Senti Moja lakini hakusahau Soka lake aliloanzia huko kwao Guinea na baadae kuendelea kuwa Kocha akiwafundisha pia Wanawe Watatu huko Roissy-en-Brie.

Mwaka 2016 alipohojiwa na Wanahabari alinena: “Nilicheza Soka Madaraja ya chini kupita nilivyotaka. Nilitaka Wanangu wacheze Madaraja ya juu, Nilikuwa mkali mno kwao walipokuwa wadogo na hilo liliwafanya wajifunze haraka. Ilifika wakati nafundisha Watoto wengine ili mradi Paul aweze kucheza akiwa na Miaka Minne, Mitano, Sita. Nilitaka wawe kiwango cha juu kabisa!”

PUMZIKA KWA AMANI, Baba yetu.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment