EPL: CHELSEA BINGWA 2016/2017

 Tokeo la picha la chelsea vs west browich image epl

Chelsea wametwaa Ubingwa wa England huko The Hawthorns baada  ya kuitungua West Bromwich Albion 1-0 katika Mechi ya EPL, LIGI KUU ENGLAND, kwa Bao la Dakika ya 82 la Michy Batshuayi alietokea Benchi.

Chelsea sasa wanaongoza Ligi hii wakibakisha Mechi 2 na wana Pointi 87 kwa Mechi 36 ambazo haziwezi tena kufikiwa na Timu ya Pili Tottenham Hotspur ambao wana Pointi 77 kwa Mechi 35.

Batshuayi, Mchezaji kutoka Belgium mwenye Miaka 23, alikuwa hajaifungia Chelsea tangu Agosti, aliingizwa Dakika ya 76 kumbadili Pedro na kuseleleka kuunganisha Pasi ya Cesar Azpilicueta na kufunga Bao lililoipa Chelsea Ubingwa chini ya Meneja Mpya wa Msimu huu Mtaliana Antonio Conte.

@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@
JE WAJUA?
  • Chelsea wametwaa Taji la 6 la Ubingwa England na la 5 kwenye zama hizi za EPL, Ligi Kuu England. Timu pekee iliyotwaa Mataji mengi ya Ubingwa England ya EPL ni Manchester United yenye Mataji 13 ya EPL na 20 kwa Ujumla.
  • Antonio Conte ni Meneja wa 4 kutoka Italy aliewahi kutwaa Ubingwa wa England kufuatia Carlo Ancelotti, Roberto Mancini na Claudio Ranieri.
@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@

Sasa kibarua kinachofuata ni cha Antonio Conte kumuiga alichofanya Carlo Ancelotti Mwaka 2010 alipotwaa Dabo katika Msimu wake wa kwanza na Chelsea kwa hapo Mei 27 kwa kuifunga Arsenal Wembley katika Fainali ya FA CUP.

Kwenye Mechi nyingine ya EPL iliyochezwa Jana huko Goodison Park, Everton pia iliitungua Watford 1-0 kwa Bao la Dakika ya 56 la Ross Barkley Mchezaji ambae amegoma kusaini Mkataba Mpya akishinikiza kuhama.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment