SIMBA YAPAA KILELENI KWA MASAA

   Tokeo la picha la simba image vpl vs stand united

SIMBA wanaongoza VPL, Ligi Kuu Vodacom, baada ya jana kuifunga Stand United 2-1 kwenye Mechi iliyochezwa Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.
 
Suleiman Kassim ‘Selembe’ aliipa Stand United Bao kabla hata Dakika 1 kutimia lakini JumaLuizio akaipigia Simba Bao 2 Dakika za 24 na 34 na kuipa ushindi wa 2-1.

Ushindi huo wa jana umeiweka Simba kileleni mwa VPL wakiwa na Pointi 65 kwa Mechi 29 wakibakisha Mechi tu.

Lakini uongozi huo wa Simba huenda ukafutwa leo Jumamosi ikiwa Mabingwa Watetezi Yanga wataifunga Mbeya City kwenye Mechi itakayochezwa Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.

Yanga wapo Nafasi ya Pili wakiwa na Pointi 62 kwa Mechi 27 wakibakiza Mechi 3.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment