UEFA EUROPA LIGI: FAINALI NI MAN UNITED NA AJAX..

 Tokeo la picha la MAN U VS CELTA VIGO IMAGE

Manchester United na Ajax Amsterdam zimetinga Fainali ya UEFA EUROPA LIGI baada kupeta Mechi zao za Marudiano za Nusu Fainali.
 
Man United walitoka Sare 1-1 na Celta Vigo na wao kusonga kwa Jumla ya Bao 2-1 kwa vile walishinda 1-0 Wiki iliyopita huko Spain wakati Ajax wamefungwa 3-1 lakini wamesonga kwa Jumla ya Bao 5-4 baada ya kushinda Mechi ya Kwanza 4-1.

Man United walitangulia kufunga Dakika ya 17 kwa Bao la Kichwa la Marouane Fellaini alipounganisha Krosi ya Marcus Rashford.

Celta Vigo walisawazisha Dakika ya 86 kwa Bao la Kichwa la Fancundo Roncaglia.

Dakika chache baada ya Bao hilo la kusawazisha, Refa aliwatoa kwa Kadi Nyekundu Eric Bailly wa Man United na Roncaglia kwa kuvaana.

          Exultations from Manchester United’s manager Jose Mourinho.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment