AFCON 2017 MABINGWA WATETEZI WATUPWA NJEE.

Tokeo la picha la IVORY COAST NATIONAL TEAM IMAGE

MECHI za mwisho za Kundi C la AFCON 2017, Mashindano ya 31 ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, zimekamilika Usiku wa kuamkia leo huko Gabon na Mabingwa Watetezi Ivory Coast kutupwa nje baada kuchapwa 1-0 na Morocco ambao wametinga Robo Fainali pamoja na Congo DR iliyoibandika Togo 3-1.
 
Mfungaji Bora wa AFCON 2017, Junior Kabananga, ndie aliefunga Bao la kwanza kwa Congo DR na wakafuata Mubele na M’Poku na Bao la Togo kuingizwa na Kodjo Fo-Doh Laba.
 Tokeo la picha la Junior Kabananga IMAGE

Kwenye Mechi ya Morocco na Ivory Coast, Bao la ushindi la Morocco lilifungwa Dakika ya 64 na Rachid Alioui kwa kigongo cha Mita 25 na kumweka kidedea Kocha wao Herve Renard ambae ndie aliiongoza Ivory Coast kutwaa Ubingwa huu Mwaka 2015. 

Jumatano Usiku Mechi za mwisho za Kundi D ambazo ndizo za mwisho kabisa za Makundi zitachezwa huku Ghana wakiwa tayari washafuzu Robo Fainali na kuiacha ngoma iwe kwa Egypt na Mali nani kuungana nao wakati Uganda wakiwa tayari wametupwa nje.

MSIMAMO:

AFCON-JAN25
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment