BENZEMA AIPELEKA REAL MADRID ROBO FAINALI YA COPA DEL REY.

Tokeo la picha la BENZEMA IMAGE
BAO la BENZEMA la dakika ya 90 na ushei limesaidia Real Madrid kupata suluhu ya 3-3 walipocheza Ugenini na Sevilla katika Mechi ya Pili ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya Copa del Rey na kutinga Robo Fainali kwa Jumla ya Bao 6-3 kwa Mechi 2 lakini pia kuweka Rekodi huko Spain ya kutofungwa katika Mechi 40.
 
Wakiwa wameshinda 3-0 huko kwao Santiago Bernabeu wakicheza bila ya Masta wao kadhaa akiwemo pia Mchezaji Bora Duniani Cristiano Ronaldo Usiku huu pia huko walicheza bila ya hao.
 Tokeo la picha la BENZEMA IMAGE

Real walijikuta wako nyuma 1-0 katika Dakika ya 10 baada ya Danilo kujifunga na kusawazisha Dakika ya 48 kwa Bao la Marco Asensio lakini wakajikuta wako 3-1 nyuma kwa Bao za Sevilla zilizofungwa Dakika za 53 na 77 na Jovetic na Iborra.
Kepteni Sergio Ramos aliipa Real Bao la Pili Dakika ya 83 na Karim Benzema, alieingizwa mwishoni, kusawazisha Dakika ya 93.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment