RAHA ZA EPL ZAREJEA TENA WIKIENDI HII.

Tokeo la picha la epl image

BAADA YA KUSIMAMA KWA EPL tangu Januari 4 wakati Tottenham Hotspur ilipowatandika Vinara wa EPL, Ligi Kuu England, Chelsea Bao 2-0, Ligi hii inarejea tena Wikiendi hii.
 
Mechi ya kwanza kabisa ni Jumamosi huko White Hart Lane ambako Spurs, walio Nafasi ya 3 wakiwa Pointi 2 nyuma ya Timu ya Pili Liverpool na 7 nyuma ya Chelsea, watacheza na West Bromwich Albion walio Nafasi ya 8.
Tokeo la picha la spurs vs west bromwhich match preview image

Kisha Siku hiyo hiyo Jumamosi zitafuata Mechi 6 zote zikianza Saa 12 Jioni na kati ya hizo ni ile ya Swansea City, ambao wako Nafasi 1 toka mkiani, kuwakaribisha Arsenal walio Nafasi ya 5 wakiwa Pointi 8 nyuma ya Vinara Chelsea.

Siku hiyo, Mechi ya mwisho ni Usiku huko King Power Stadium ambako Mabingwa Watetezi Leicester City watacheza na Chelsea ambao ndio wanaongoza Ligi na ndio kwanza wakitoka kwenye kipigo cha 2-0 toka kwa Spurs.
 Tokeo la picha la Leicester City v Chelsea  preview image

Jumapili zipo Mechi 2 ikianza ile ya Goodison Park kati ya Everton, walio Nafasi ya 7, na Man City ambao wako Nafasi ya 4.
 Tokeo la picha la Everton v Manchester City image

Kisha utafuata mtanange huko Old Trafford wakati Man United ambao wapo kwenye wimbi la kushinda Mechi 9 mfululizo wakicheza na Mahasimu wao wa Jadi Liverpool.

Tokeo la picha la Manchester United v Liverpool image

Wimbi hili la ushindi kwa Man United ni refu tangu Msimu wa 2008/09 waliposhinda Mechi 11 mfululizo kati ya Januari na Februari na kuelekea kutwaa Ubingwa wa England na Kombe la Ligi wakiwa chini ya Meneja Lejendari Sir Alex Ferguson.

EPL – Ligi Kuu England Ratiba
++Saa za Bongo++  
Jumamosi Januari 14

1530 Tottenham vs West Bromwich Albion 
    
1800 Burnley vs Southampton  
             
1800 Hull City vs Bournemouth
              
1800 Sunderland vs Stoke City 
              
1800 Swansea City vs Arsenal  
              
1800 Watford vs Middlesbrough
             
1800 West Ham United vs Crystal Palace  
         
2030 Leicester City vs Chelsea 
               
Jumapili Januari 15

1630 Everton v Manchester City 

1900 Manchester United v Liverpool
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment