SIR ALEX ASEMA: “HAKUNA ATAEVUNJA REKODI YA ROONEY!”

Tokeo la picha la sir alex furgusson image

LEJENDARI wa Manchester United Sir Alex Ferguson ametamka kuwa Rekodi ya Wayne Rooney ya kuifungia Klabu hiyo Mabao 250 haitavunjwa.
 
Rooney, mwenye Miaka 31, alifunga Bao lake la 250 kwa Klabu yake Manchester United Jumamosi iliyopita katika Dakika ya 94 walipotoka 1-1 na Stoke City huko Britannia Stadium kwenye Mechi ya EPL, Ligi Kuu England.

Bao hilo lilivunja Rekodi ya Mfungaji Bora katika Historia ya Man United, Sir Bobby Charlton, aliyoishikilia kwa Miaka 44.

Mwaka Jana, Rooney pia aliivunja Rekodi ya Sir Bobby Charlton na kuwa Mfungaji Bora katika Historia ya Timu ya Taifa ya England.
 
Sir Alex Ferguson, ambae alikuwa Meneja wa Man United tangu 1986 hadi 2013 na ambae pia ndie aliemchukua Roooney Mwaka 2004 kutoka Everton, ameeleza: “Rekodi ilidumu Miaka 44 na wakati Rooney anajiunga sikutegemea kama atavunja Rekodi ya Sir Bobby! Kufanya hilo ni kitu kikubwa. Ni ajabu! Yeye amecheza kama Gemu 200 chini ya zile za Sir Bobby. Na hilo ni ajabu zaidi!”

Aliongeza: ‘Sidhani kama kuna Mtu atampita Rooney. Siwezi kusema hapana, hapana usiseme hapa, lakini ukitizama Soka la sasa, Man United ni moja ya Klabu chache kabisa kuweka Mchezaji kwa Miaka 10!”

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment